TanzMED yazindua huduma za afya kidigitali 

By Mwandishi Wetu , Nipashe
Published at 05:15 PM Jul 23 2024
Wafanyakazi wa applikesheni mpya ya afya ya TanzMED wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi wa applikesheni hiyo. 
Picha: Mpigapicha Wetu
Wafanyakazi wa applikesheni mpya ya afya ya TanzMED wakiwa kwenye picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi wa applikesheni hiyo. 

KAMPUNI ya TanzMED imezindua rasmi applikesheni mpya ya afya inayolenga kumuezesha Mtanzania kupata taarifa na huduma bora za afya moja kwa moja kupitia simu yake ya mkononi kwa lugha ya Kiswahili.

Akizungumza katika uzinduzi huo jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi na Mwanzilishi wa TanzMED , Mkata Nyoni, amesema  App hiyo inapatikana kwenye App Store na Google Play, ambapo unaweza kuipakua na kujisajili bila gharama yoyote na kufurahia huduma mbalimbali zinazotolewa ikiwa inawezeshwa na akili mnemba (AI).

Amesema kupitia TanzMED, mtu anaweza kuzungumza na Madaktari Bingwa kwa njia ya video au kuchat. Pia, ataweza kupata huduma za afya ya akili kwa ushirikiano na Hospitali ya Taifa ya Afya ya Akili ya Mirembe, pamoja na nyenzo za afya ya wanawake, ikijumuisha afya ya uzazi na hedhi.

 Aidha, Mtanzania anaweza kupata elimu kuhusu Ukimwi/VVU na huduma nyingine za afya, na kuweka miadi ya kukutana na daktari pamoja na kufika hospitali iliyo karibu na wewe.

“Lengo kubwa la kuanzisha TanzMED  ni kuwawezesha Watanzania kuwa na afya bora kwa kukuleta huduma mbalimbali za afya kiganjani mwako. Pia, TanzMED  inakuwezesha kuweka miadi na hospitali pamoja na kufika hospitali iliyo karibu na sehemu uliopo,” alisema Nyoni.

Tunatumia fursa hii kuwakaribisha Watanzania wote kutembelea Google Play na App Store na kupakua app ya TanzMED  bure kabisa na kufurahia huduma za afya kidigitali!.