KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk.Emmanuel Nchimbi, amempa muda hadi mwishoni mwa mwezi huu, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, kumaliza tatizo la fedha za kujikimu (Boom) kwa wanafunzi wa Chuo cha Ustawi wa Jamii Tengeru, ambao wana miezi sita hawajapata.
Agizo hilo limetolewa leo baada ya Mwanafunzi wa Chuo cha Ustawi wa Jamii Tengeru, mkoani Arusha, Digna Nasari, ambaye pia ni Katibu Mwenezi wa CCM Kata ya Ambureni, kumweleza katibu mkuu huyo kuwa mpaka sasa ni mwezi wa sita wanachuo chuoni hapo hawajapata 'Boom'.
Akizungumza na wananchi wa USA-River, Wilaya ya Meru, mkoani hapa, Balozi Nchimbi ambaye amehitimisha ziara yake Arusha na kuelekea Mkoa wa Kilimanjaro, amemwelekeza Waziri wa Elimu kwamba, tatizo hilo liishie ifikapo mwishoni mwa mwezi huu.
© 2024 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED