WB yatoa bil 230/- ujenzi vituo Haki Jumuishi

By Christina Haule , Nipashe
Published at 06:09 PM Feb 06 2025
Mtendaji Mkuu wa Mahakama, Profesa Elisabte Ole Gabriel akizungumza kuhusu utekelezaji wa bajeti ha mahakama ya haki jinai katika kipindi cha robo mwaka 2024/25.
Picha: Christina Haule
Mtendaji Mkuu wa Mahakama, Profesa Elisabte Ole Gabriel akizungumza kuhusu utekelezaji wa bajeti ha mahakama ya haki jinai katika kipindi cha robo mwaka 2024/25.

MAHAKAMA ya Tanzania, imepokea dola za milioni 90 sawa na Sh. bilioni 230, zitakazotumika katika kukamilisha ujenzi wa mahakama tisa za Haki Jumuishi nchini.

Hatua hiyo ni mafanikio ya kusikilizwa na kumalizika kwa mashauri 2000, kwa mwaka 2024/25 ambayo ni sawa na asilimia 98.5.

Mtendaji Mkuu wa Mahakama, Prof. Elisante Ole Gabriel, amesema hayo leo, wakati akiongea na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa bajeti ya mahakama na majukumu kwa nusu ya mwaka wa fedha 2024/25.

Prof. Ole Gabriel, amesema fedha hizo zimetokana na manufaa yaliyojitokeza wakati wa utekelezaji wa vituo sita vya Haki Jumuishi nchini na kwamba fedha hizo zilizotolewa na Benki ya Dunia (WB), 

Waandishi wa habari wakifuatilia taarifa inayotolewa na Mtendaji Mkuu wa Mahakama, Profesa Elisante Ole Gabriel.
“Fedha zitasaidia katika ujenzi wa vituo jumuishi vingine tisa kwenye mikoa tisa nchini, ambayo ni mikoa ya Katavi, Simiyu, Songwe, Ruvuma, Geita, Lindi, Njombe Singida na Pemba,” amesema.

Akizungumzia utendaji wa vituo hivyo vya mahakama na Haki Jumuishi, Msaidizi wa Mawakili wa Kujitegemea, Ivan Calvin, anasema maboresho hayo ya mahakama kupitia vituo vya Haki Jumuishi na mahakama zinzotembea, yametoa hamasa ya ufanyaji kazi na kuwapo kwa huduma za kidigitali kumeepusha gharama na upatikanaji huduma ni haraka kwao na kwa wananchi.