Watoto watatu wa familia moja mkoani Shinyanga wamefariki dunia usiku wa kumakia leo, Ijumaa Aprili 26,2024 baada ya kuangukiwa na nyumba walimo kuwa wamelala.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mwenyekiti wa Kitongoji Cha Miembeni B, Kata ya Mwantini, Masai Senema, inasema kuwa Watoto hao ni wa familia ya Ngasa Mataluma.
Amesema kuwa tukio hilo limetokea baada ya nyumba hiyo waliyokuwa wamelala na mama yao Kashinje Nchembi kuanguka kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.
© 2024 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED