Ajali iliyohusisha mabasi mawili na lori yaua wawili

By Mwandishi Wetu , Nipashe
Published at 11:31 AM Mar 28 2024
Ajali iliyohusisha mabasi mawili na lori.
PICHA: EATV
Ajali iliyohusisha mabasi mawili na lori.

WATU wawili wamefariki dunia na wengine kujeruhiwa kwenye ajali ya barabarani iliyohusisha magari matatu ambayo ni Basi la Kampuni ya New Force na Kampuni ya Sauli pamoja na lori la mafuta.

Ajali hiyo imetokea leo Machi 28, 2024 majira ya alfajiri katika eneo la Mlandizi mkoani Pwani. 

Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Aboubakar Kunenge amefika katika eneo la tukio na kudhibitisha vifo vya watu hao, huku zoezi la kumwaga mafuta kwenye lori ili lisilete madhara zaidi likiendelea kufanywa na Jeshi la Zimamoto.