SBL, NCT washirikiana kukuza ujuzi wa wanafunzi wa ukarimu

By Mwandishi Wetu , Nipashe
Published at 07:49 PM Sep 30 2024
SBL, NCT washirikiana kukuza ujuzi wa wanafunzi wa ukarimu
Picha:Mpigapicha Wetu
SBL, NCT washirikiana kukuza ujuzi wa wanafunzi wa ukarimu

Zaidi ya wanafunzi 100 wa ukarimu watanufaika na fursa za mafunzo zilizoboreshwa ambazo zitazidi kuimarisha sekta inayokua kwa kasi ya utalii na ukarimu nchini Tanzania.

Kampuni ya Serengeti Breweries Limited (SBL) imesaini hati ya makubaliano (MoU) na Chuo cha Taifa cha Utalii (NCT) katika kupiga hatua muhimu katika kuboresha mafunzo ya ujuzi wa ukarimu. Ushirikiano huo unalenga kuwapa wanafunzi na wahitimu wa ukarimu ujuzi muhimu na uzoefu wa vitendo ili kuchochea fursa ya ajira na kuchangia ukuaji endelevu wa sekta za utalii na ukarimu nchini.

Ushirikiano huo ni sehemu ya programu ya SBL "Learning for Life," ambayo ni mpango chini ya ajenda yake pana ya ustawi "Spirit of Progress" iliyoundwa ili kuboresha maisha na kuunda fursa za ajira kwa vijana wa Kitanzania. Kupitia programu hii, wanafunzi wa chou cha Taifa cha utalii watapata mafunzo maalum katika ujuzi wa biashara na ukarimu, ikiwa ni pamoja na mawasiliano, uongozi, kujitambua, upangaji bajeti, na usimamizi wa muda. Aidha, wanafunzi watapata uzoefu wa vitendo katika shughuli za ukarimu kupitia mafunzo kwa vitendo na mafunzo ya ndani.

Akizungumza kuhusu ushirikiano huo, John Wanyancha, Mkurugenzi wa Mahusiano wa SBL, alisisitiza kujitolea kwa kampuni hiyo katika kuwawezesha vijana: “Tunafurahia kushirikiana na Chuo cha Taifa cha Utalii ili kuunda njia kwa vijana kufanikiwa katika sekta ya ukarimu. Programu yetu ya “Learning for Life” siyo tu kuhusu elimu; inahusu kutoa ujuzi wa maisha halisi ambao utawasaidia wanafunzi hawa kupata ajira yenye maana na kuchangia ukuaji wa sekta ya utalii nchini Tanzania.”

Kupitia ushirikiano huu, SBL itasaidia kutoa mafunzo kwa wanafunzi wa NCT katika sekta ya ukarimu, kuwapa fursa ya kujifunza kwa vitendo. Kampuni hiyo pia itatoa mtaala wa Learning for Life unaolenga maeneo muhimu ambayo yanaongeza ajira na kuandaa wanafunzi kwa ajili ya kazi yenye mafanikio katika sekta ya ukarimu.

Naye Dk. Florian Mtey, Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Utalii, alisifu ushirikiano huo kama fursa ya mabadiliko kwa wanafunzi: “Ushirikiano huu na SBL utaimarisha sana uzoefu wa kujifunza kwa wanafunzi wetu kwa kuchanganya maarifa ya nadharia na uzoefu wa vitendo wa sekta. Ujuzi na mafunzo ya vitendo watakayopata kupitia programu hii yatawaandaa kukidhi mahitaji ya sekta ya ukarimu na utalii nchini Tanzania.”

Mbali na mafunzo ya ndani, SBL itaandaa programu za Mafunzo ya Wakufunzi kwa wakufunzi wa chou hicho waliochaguliwa ili kuwasaidia kufundisha mtaala wa Learning for Life. Ushirikiano huu utaendelea nje ya darasa, ambapo SBL itasaidia mafunzo ya wanafunzi katika Diageo Bar Academy, ikiwemo mafunzo ya mchanganyiko wa vinywaji na ujuzi mwingine wa vitendo muhimu kwa mafanikio katika sekta ya ukarimu.

Hati hiyo ya makubaliano inaeleza ushirikiano wa miaka miwili ambapo SBL na NCT watafanya kazi kwa karibu kufuatilia maendeleo ya wanafunzi, kutoa mrejesho, na kusaidia maendeleo yao. SBL pia itasaidia sherehe za wahitimu na uzinduzi wa vyombo vya habari ili kukuza mafanikio ya mpango huo.

Kama sehemu ya maono yake ya muda mrefu ya ustawi, SBL imejitolea kusaidia jamii za ndani na kuchangia maendeleo ya kitaifa. Ushirikiano huu unaendana na juhudi za kampuni hiyo kuwawezesha vijana wa Kitanzania kwa kuwapa ujuzi na rasilimali zinazohitajika ili kufanikiwa katika sekta inayobadilika ya ukarimu.

6