Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Anthony Mtaka amesema kuna kila sababu ya kuendelea kukuza vipaji vya watoto kupitia mpira wa miguu kwa sababu hivi ni biashara ambayo inazalisha mabilionea.
Mtaka ameeleza hayo mjini Njombe wakati akipokea mipira 1,000 iliyotolewa na shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF) kwa ajili ya shule za msingi.
Aidha Mtaka ameongeza kuwa, kwa sasa katika mapinduzi ya nne ya viwanda, dunia inashuhudia michezo ikizalisha mabilionea na matilionea.
"Kwenye mapinduzi ya nne viwanda karne ya 21, dunia inashuhudia michezo ikizalisha matajiri na mabilionea na football ikiwa ni mchezo mama unaoongoza kuzalisha ajira na wafanyabiashara wakubwa," amesema Mtaka.
© 2024 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED