RAIS Samia Suluhu Hassan, amempongeza Bassirou Diomaye Faye kwa kuchaguliwa kuwa Rais mteule wa Jamhuri ya Senegal.
Rais Samia ametoa pongezi hizo kupitia ukurasa wake wa Instagram, huku akisema kuwa wataendelea kufanya kazi pamoja ili kuimarisha uhusiano kati ya Tanzania na Senegal
“Nawasilisha pongezi zangu za dhati kwa Rais Mteule wa Jamhuri ya Senegal, Bassirou Diomaye Faye, kwa ushindi ulioupata katika uchaguzi wa urais wa 2024 wa Senegal; na ninawapongeza watu wa Senegal kwa uchaguzi huo wa amani. Na ninatarajia kufanya naye kazi tukiimarisha uhusiano kati ya nchi zetu.”
© 2024 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED