Vikundi 100 wanawake kunolewa elimu ubunifu

By Pilly Kigome , Nipashe
Published at 04:04 PM Feb 10 2026
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Dar es Salaam Amina Amo
Picha: Mpigapicha Wetu
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Dar es Salaam Amina Amo

Zaidi ya vikundi 100 vya wanawake kutoka Mkoa wa Dar es Salaam vitapata mafunzo ya uwezeshwaji kiuchumi, ili kuongeza tija uelewa na ubunifu katika shughuli zao.

Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Dar es Salaam,  ambae pia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Amo, Amina Said, amesema mafunzo yatawalenga makundi yote ya wanawake yanayofanya shughuli za kiuchumi, ili waweze kujiongezea kipato.

Mafunzo hayo yanatarajiwa  kufunguliwa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Halima Mamuya.