Taasisi tano zapewa vyeti utekelezaji sheria PSSSF

By Mwandishi Wetu , Nipashe
Published at 07:20 PM Feb 10 2026
Watunukiwa vyeti vya umahiri katika utekelezzaji wa Sheria ya Mfuko wa PSSSF
Picha: Mpigapicha Wetu
Watunukiwa vyeti vya umahiri katika utekelezzaji wa Sheria ya Mfuko wa PSSSF

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Deus Sangu, amezitunuku taasisi tano za umma vyeti vya umahiri kwa kuzingatia na kutekeleza Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), katika Mkutano wa Wadau wa Sekta ya Kinga ya Jamii uliofungwa Februari 10, 2026 jijini Arusha.

Akizitaja taasisi hizo, Mkurugenzi wa Uendeshaji wa PSSSF, Mbaruku Magawa, amesema ni Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Benki ya Taifa ya Biashara (NBC Limited), NMB Plc, Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Magawa amesema vyeti hivyo vimetolewa kutokana na umahiri wa taasisi hizo katika kuwasilisha michango kwa wakati, kutoa taarifa sahihi za wanachama na kuwasilisha madai kwa njia ya mtandao kwa kuzingatia sheria za mfuko.

Mkutano huo, ambao pia ulihusisha uzinduzi wa Sera ya Taifa ya Kinga ya Jamii, umefungwa rasmi na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete.