NCAA yawaita hifadhini wanawake 800 kuona 'big 5'

By Godfrey Mushi , Nipashe
Published at 12:11 PM Feb 24 2025
NCAA yawaita hifadhini wanawake 800 kuona 'big 5'
Picha:Mpigapicha Wetu
NCAA yawaita hifadhini wanawake 800 kuona 'big 5'

ZAIDI ya wanawake 800 kutoka maeneo mbalimbali nchini, watayatumia maadhimisho ya siku ya wanawake duniani, kufanya utalii wa ndani katika vivutio vya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA).

Maadhimisho hayo yatakayofanyika mkoani Arusha, Machi 8 mwaka huu, yataongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan. 

Jana, Kamishina Mwandamizi Msaidizi wa Huduma za Utalii na Masoko wa NCAA, Mariam kobelo, alisema safari hiyo inatarajia kufanyika Machi 7 mwaka huu, ambayo ni siku moja kabla ya maadhimisho hayo. 

Alisema kuwa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, imeandaa safari kwa wanawake waliopo ndani na nje ya  mkoa wa Arusha, kwa lengo la kuwapa motisha wanawake wawe na utaraibu wa kutembelea hifadhi zao pamoja na kuunga mkono juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan za kutangaza utalii wa ndani. 

"Rais amekuwa kinara wa kuutangaza utalii  kupitia filamu mbili ya Tanzania, The Royal Tour pamoja na Amazing Tanzania. Sisi kama wanawake katika uhifadhi na utalii tunaziunga mkono juhudi zake, kwa kuwahamasisha wanawake wote waweze kutembelea hifadhi," alisema Mariam kobelo.

Aidha, alisema wanawake katika mamlaka hiyo  wameandaa  shughuli nyingine za kimaendeleo katika maadhimisho hayo ni pamoja na kufanya usafi katika barabara wanazopita watalii pamoja na kurejesha shukrani  kwa jamii  ikiwemo tumbelea wagonjwa waliopo hospitalini kuwapa faraja vijana. 

Kwa upande wake, Mkugenzi Mtendaji wa Kampuni yaTanzanite Coparates, Elina Mwangomo, alisema kuwa   kampuni yake ndio imeanda ziara hiyo kwa kuahirikiana na mamlaka ya hifadhi ha ngiringiro ambapo safari  itagharimu Sh. 170,000 kwa ajili ya  usafiri ,kingilio, kofia ,chai ,chakula cha mchana pamoja  fedha za waongoza watalii.