Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), imetangaza bei kikomo za bidhaa za mafuta ya Petroli hapa nchini zitakazotumika kuanzia leo Jumatano tarehe 05 Februari 2025 saa 6 usiku, kwa mwezi Februari 2025 bei za rejareja na jumla.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, bei ya petroli kwa rejareja katika Jiji la Dar es Salaam imeongezeka kwa asilimia 0.957, dizeli kwa asilimia 2.18 na mafuta ya taa kwa asilimia 1.25.
Hii ikiwa na maana kuwa sasa wanunuzi wa mafuta kwa bei ya rejareja katika Jiji la Dar es Salaam watanunua lita moja kwa Sh2, 820 kwa petroli, dezeli Sh2, 703 na mafuta ya taa kwa Sh2, 710.
Bei hizo ni kutoka Sh2, 793 kwa bei ya petroli ndani ya jiji la Dar es Salaam kwa Januari mwaka huu, dizeli Sh2, 644 na mafuta ya taa kwa Sh2, 676.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED