JESHI la Polisi Mkoa wa Geita, linawashikilia watu watatu wa familia moja kwa tuhuma ya mauaji ya baba yao mzazi Hussein Bundala, mwenye umri wa miaka 103.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Geita, Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Safia Jongo amebainisha hayo Februari 24, mwaka huu, wakati akizungumza na vyombo vya habari mkoani hapo.
Aidha amesema uchunguzi wa awali unaonesha marehemu aliuwawa kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali sehemu za kichwani, usoni na shingoni.
“Jeshi la polisi linaendelea kukamilisha uchunguzi wa tukio hili kwa kushirikiana na taasisi nyingine za ulinzi na usalama ili watuhumiwa wafikishwe mahakamani kujibu tuhuma hizo,” amesema Jongo.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED