Marekani yajiandaa na operesheni kijeshi dhidi ya Iran

By Mwandishi Wetu , Nipashe Jumapili
Published at 01:27 PM Feb 15 2026
Rais wa Marekani, Donald Trump (kulia) na Kiongozi Mkuu wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei,
Picha: Mtandao
Rais wa Marekani, Donald Trump (kulia) na Kiongozi Mkuu wa Iran, Ayatollah Ali Khamenei,

Shirika la habari la Reuters liliripoti, likiwanukuu maafisa wawili wa Marekani, kwamba jeshi la nchi hiyo linajiandaa kwa operesheni inayowezekana dhidi ya Iran ndani ya wiki kadhaa ikiwa Rais Donald Trump, ataamuru shambulio.

Operesheni hiyo, inaweza kugeuka kuwa mzozo mkubwa zaidi kuliko ilivyotokea hapo awali kati ya nchi hizo mbili.

Kufichuliwa kwa habari hii na maafisa ambao hawakutaka kutajwa jina kutokana na hali nyeti ya upangaji huu kunaleta hatari kwa mazungumzo yanayoendelea ya Marekani na Iran.

Iran na Marekani zilifanya duru ya kwanza ya mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja mjini Muscat, mji mkuu wa Oman, Ijumaa iliyopita.

Shirika la habari la Reuters liliripoti, likiwanukuu maafisa hao wawili wa Marekani, kwamba mipango inayoendelea wakati huu ni ya kiwango cha juu zaidi kuliko hapo awali, na mmoja wa maafisa alisema kuwa katika operesheni endelevu, jeshi la Marekani linaweza kushambulia serikali ya Irani na vifaa vya usalama, sio tu miundombinu ya nyuklia.

Marekani ilitangaza siku ya Ijumaa kuwa inapeleka shehena kubwa zaidi ya ndege kwa kutumia meli ya kubeba ndege za kivita ya Gerald R. Ford, Mashariki ya Kati.

Gerald R. Ford itaungana na USS Abraham Lincoln, ndege kadhaa za kivita, ndege za kivita na ndege za uchunguzi ambazo zimetumwa Mashariki ya Kati katika wiki za hivi karibuni.

Trump asema mabadiliko ya utawala wa Iran yanaweza kuwa 'jambo bora'

Kutoka bunduki hadi mapanga: Silaha zilizoua maelfu ya raia nchini Iran

Mshirikishe mwenzako, Reuters: Wanajeshi wa Marekani wanajiandaa kwa operesheni inayowezekana ya wiki moja dhidi ya Iran

Chanzo: BBC