HALMASHAURI ya Ushetu mkoani Shinyanga, imebuni mbinu mpya ya kuongeza ufaulu kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari, kwa kutoa motisha na vyeti vya pongezi kwa walimu wa masomo na shule zinazofanya vema kwenye mitihani ya mwisho.
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anamringi Macha ndiye aliyekabidhi vyeti vya pongeza na fedha taslimu, kwa walimu waliofanya vema kwenye masomo kutoka shule 10 bora wakati kikao cha tathimini ya elimu ya msingi na sekondari kilichofanyika Kata ya Nyamilangono na jumla ya walimu 1,228 walihudhuria.
Amesema vyeti hivyo, vikaongezee morari ya kufundisha, ili kuhakikisha wanaondoa sifuri katika mitihani ya darasa la nne na kidato cha tano, kwa kuwa baadhi ya wanafunzi wanakatishwa tamaa ya uwapo wa kazi shuleni zisizoendana na umri wao.
Amewataka walimu kutokukata tamaa ya kupambana na utoro, kwa wanafunzi na badala yake wawahamasishe wanafunzi wapende masomo, ili kama kuna mzazi atabainika kumshawisha mtoto kuolewa au kuchunga mifugo wataweza kupata taarifa na kuchukua hatua za haraka.
Mkuu wa Divisheni ya Elimu Msingi, Zelena Ntulo, amesema vyeti vya pongezi na fedha vinataolewa kwa Mshindi wa Taalumu Shuleni, kwa shule 10 bora, Mabingwa wa Somo kwa kila somo, shule zilizoongeza ufaulu na Usimamizi Bora wa Miradi ya Shule kwa kuzingatia matumizi sahihi ya fedha na ubora wa majengo.
Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Hadija Kabojela, amesema utaratibu huo waliona ni njia ya kuongeza ufaulu kwa wanafunzi hasa wa kike ambao wamekuwa wakikatisha masomo, kwa sababu mbalimbali ikiwamo utaro.
Amesema, tathimini waliyofanya kabla ya kutoa vema itaongeza ufaulu kwa wanafunzi na kupunguza ufaulu wa wastani wa divisheni nne na sifuri, kwa kuwa miaka ya nyuma walikuwa na sifuri 300 katika shule za msingi na sekondari na sasa zimebaki 47 ambazo nazo wanapambana kuziondoa.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED