Dorothy :Tutashirikiana na vyama makini kupambania demokrasia

By Enock Charles , Nipashe Jumapili
Published at 02:52 PM Feb 23 2025
Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Dorothy Semu
PICHA:MTANDAO
Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Dorothy Semu

Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Dorothy Semu amesema yupo tayari kuongoza mapambano ya kupigania demokrasia nchini kwa gharama yoyote kwa kushirikiana na vyama vingine.


Akizungumza katika kikao cha Halmashauri Kuu cha chama hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Hakainde Hichilema jijini Dar es Salaam, kiongozi huyo amesema kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka huu mambo siyo rahisi hivyo kuahidi kushirikiana na vyma vingine ili kupigania demokrasia.

“Tukielekea uchaguzi mkuu wa mwaka huu, ni muhimu kutambua kwamba kuna hujuma na hila zinazotumiwa ili kukatisha tamaa wananchi.” Amesema Dorothy

“Hali hii inatufanya tuwe na jukumu kubwa la kusukuma ajenda ya kuunda jukwaa la mapambano ya pamoja na vyama makini. Tunahitaji kufanya shughuli za pamoja ili kuimarisha umoja wetu wenye nguvu utakao leta tija ya mabadiliko.” Amesema 

“Tunahitaji kupambania kuurejesha uchaguzi huru. Nchi yetu hasa hakuna uchaguzi, tuna uchafuzi. Tutaunganisha nguvu na vyama vyote makini na wadau wa demokrasia nchini.”