Rais Samia azindua Shule ya Sekondari ya Wasichana Tanga

By Hamida Kamchalla , Nipashe
Published at 02:43 PM Feb 25 2025
Rais Samia Suluhu leo Februari 25,2025 amezindua Shule ya Sekondari ya Wasichana Mkoa wa Tanga iliyopo Wilaya ya Kilindi ikiwa ni sehemu ya ziara ya kikazi mkoani humo.
Picha:Ikulu
Rais Samia Suluhu leo Februari 25,2025 amezindua Shule ya Sekondari ya Wasichana Mkoa wa Tanga iliyopo Wilaya ya Kilindi ikiwa ni sehemu ya ziara ya kikazi mkoani humo.

RAIS Samia Sulluh Hassan amezindua shule ya wasichana ya Mkoa wa Tanga leo Februari 25 katika Kijiji cha Mabalanga wilayani Kilindi, ambayo inafundisha mchepuo wa sayansi.

Wakati akizindua shule hiyo Dk. Samia aliwaomba wananchi wilayani humo kuipa jina aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo, hayati Beatrice Shelukindo ambaye pia alikuwa mpambanaji wa masuala ya wanawake.

"Kwahiyo nikuombe Mkuu wa Mkoa ikikupendeza, mmuite jina hilo, na alikuwa mpambanaji hata alipokuwa kwenye kuwania nafasi ile ya ubunge" amesema.


5