Rais Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuwa Mwenyekiti wa Jukwaa la Viongozi wakuu wa nchi za Afrika na China mkutano huo unaotarajiwa kuaanza Septemba 4 hadi 6 mwaka huu nchini China.
Atashiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC).
Rais Samia atahutubia ufunguzi wa mkutano wa FOCAC.
Aidha, Rais Samia atafanya mazungumzo na Rais China, Xi Jinping na kushuhudia uwekaji saini wa hati za makubaliano ya uboreshaji wa reli ya Tazara.
Pia Rais atakutana na makampuni na wawekezaji kutoka China ili kuhamasisha uwekezaji zaidi nchini Tanzania.
© 2024 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED