WANANCHI wa Kijiji cha Tabu Hotel wamefunga barabara kuu ya Dodoma-Morogoro tangu majira ya saa 11 wakishinikiza kufika Mkuu wa Mkoa wa Morogoro bwana Adam Malima baada ya gari ya serikali aina ya Cruzer kumgonga mwanafunzi kwenye kivuko cha watembea kwa miguu na kusababisha kifo chake na gari husika kukimbia.
Wanasema hawataki alama peke yake wanataka matuta kwasababu ajali eneo hilo zimekuwa za mara kwa mara zikihusisha magari ya Serikali zikiua wananchi wakiwemo wanafunzi.
© 2024 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED