Israel yampiga marufuku António Guterres nchini humo

By Mwandishi Wetu , Nipashe
Published at 07:45 PM Oct 02 2024
 Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), António Guterres
Picha: Mtandao
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), António Guterres

WAZIRI wa Mambo ya Nje wa Israel, anasema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), António Guterres ni marufuku kuingia nchi ya Israel.

Israel Katz, anasema uamuzi huo, unakuja baada ya Guterres kutolaani shambulio la kombora la Iran dhidi ya Israel, siku ya jana.

Anamshutumu mkuu huyo wa UN, kwa kuwa mpinzani wa Israel na kutoa msaada kwa magaidi, wabakaji na wauaji.

Guterres atakumbukwa kama doa katika historia ya Umoja wa Mataifa kwa vizazi vijavyo,” anaongeza Katz.

Jana, Jumanne, mkuu huyo wa UN, alilaani kuongezeka kwa mzozo wa Mashariki ya Kati na kutoa wito wa kusitishwa kwa mapigano.

BBC