Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa, na Michezo Hamis Mwinjuma amewaagiza wataalamu kutoka wizara hiyo kufanya tathmini kuhusu ujenzi wa uwanja wa mazoezi kwaajili ya mashindano ya AFCON katika eneo la FFU, Morombo Jijini Arusha.
Waziri Mwinjuma ametoa maagizo hayo Februari, 15, 2025 wakati akizindua michuano ya Soka ya Chuga Cup 2025 baada ya ombi la Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Mrisho Gambo kuomba eneo hilo ujengwe uwanja wa kisasa kwaajili ya mazoezi wakati wa michuano ya Kombe la Mataifa Barani Afrika AFCON 2027 ambayo Tanzania ni miongoni mwa nchi mwenyeji.
"Wananchi wa Arusha wanayo kila sababu ya kuendelea kumwamini mbunge wao Gambo kwa sababu amekuwa akipigania miradi mbalimbali ya wananchi jijini humo ikiwemo wazo la kujenga uwanja wa kisasa wa mpira wa miguu tangu akiwa mkuu wa mkoa," amesema.
Aidha, ameeleza kiwa hajawahi kushuhudia kiongozi wa nchi akiungwa mkono na wananchi wa Arusha kama ilivyo kwa Rais Samia Suluhu Hassan.
Mwinjuma amesema kutokana na miradi ya maendeleo inayopelekwa na serikali Jijini Arusha ndiyo sababu ya wao kuelekeza mapenzi juu yake.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED