BINGWA Mbobezi wa Upandikizaji wa Nyonga na Magoti kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Mlonganzila. Hamis, ameelezea kuhusu upandikizaji wa marejeo wa nyonga na magoti huku akionya uzito mkubwa huathiri mwenendo wa waliopatiwa huduma hiyo, hivyo waudhibiti.
Bingwa wa Nyonga na Magoti kutoka MNH-Mloganzila, Dk. Abubakar Hamis, alisema kutokana na waliofanyiwa huduma hiyo kufanyika wakati teknolojia ikiwa duni, ndio sababu ya kufanyiwa upasuaji wa marejeo.
“Mvunjiko palipowekwa kiungo au palipounganishwa ni sababu ya marejeo. Lakini zaidi ni uzito, uzito husababisha nyonga, magoti kusagika paliporekebishwa,” alisema bingwa huyo.
Bingwa huyo amefafanua hayo jana, akieleza kuhusu kambi maalum Februari 26 hadi Machi 7, 2025.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED