KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na mitaji ya Umma (PIC) imeipongeza serikali kwa uwekezaji wenye tija na manufaa kwa maendeleo ya nchi inayofanya katika kiwanda cha uzalishaji wa bidhaa za ngozi Kilimanjaro International Leather Industries Co Ltd.
Akizungumza mara baada ya kutembelea kiwanda hicho mwenyekiti wa kamati hiyo Agustine Holle amesema kuwa kutokana na uwekezaji wenye tija waliouona utaiwezesha serikali kuongeza mapato.
Aidha amesema kiwanda hicho kitaunufaisha mkoa wa Kilimanjaro pamoja na mikoa ya jirani kwa kuboresha mfumo wa maisha ikiwemo kuongeza kipato kwa wakazi wa maeneo hayo na nje ya mkoa huo.
Mwenyekiti amebainisha kuwa wameridhika na uendeshaji wa Kiwanda hicho ambapo kitakapokamilika kwa asilimia 100 kinakwenda kutoa ajira 3,000 ambazo ni ajira za moja kwa moja na ajira nyingine zisizo za moja kwa moja ni 4,000.
Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Ridhiwani Kikwete ameihakikishia kamati hiyo kuwa ataendelea kusimamia maono ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuufanya uwekezaji huo wenye tija unakuwa endelevu kwa manufaa ya watanzania na nchi.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED