MNH-Mloganzila; Fursa wajawazito kujifungua kwenye jakuzi

By Christina Mwakangale , Nipashe
Published at 12:46 PM Feb 13 2025
Rahel Mushi na wataalam
Picha: MNH-Mloganzila
Rahel Mushi na wataalam

HOSPITALI ya Taifa Muhimbili (MNH)-Mloganzila imeanzisha huduma ya wajawazito kujifungulia katika jakuzi maalum (water birth).

Huduma hiyo inalenga inamsaidia mama kupunguza uchungu wakati wa kujifungua na kumuepusha kuchanika.

Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Uuguzi na Ukunga MNH)-Mloganzila, Dk. Debora Bukuku, anasema kuanzishwa kwa huduma hiyo ni mwendelezo wa kupanua wigo wa huduma.

Anasema  kwamba awali huduma hiyo ilipatikana katika Muhimbili Upanga pekee.“Nimefurahishwa na huduma ya kujifungua kwenye jakuzi inayotolewa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Mloganzila,” Rahel Mushi, miongoni mwa waliopata huduma hiyo.

Chumba chenye huduma ya jakuzi
Anasema amefurahishwa na huduma hiyo kwa kuwa wataalam walikuwa wanampatia mazoezi wakati wote akiwa kwenye jakuzi na kumfanya asihisi maumivu, hivyo anawashauri akinamama wengine kutumia huduma hiyo.

Muuguzi Mkunga Bingwa na Mtaalam wa kusaidia kinamama kujifungua kwenye jakuzi hospitalini hapo, Rwehabura France, amesema miongoni mwa faida za mama kujifungulia kwenye jakuzi, ni ndugu atayemchagua.“Fursa ni kukaa na wataalam na kukaa naye kwa muda wote atakaokuwa kwenye jakuzi, kitu ambacho kitamuongezea  faraja zaidi na kutohisi maumivu,” anasema mtaalamu huyo.

Chumba chenye huduma ya jakuzi
France ameongeza kuwa kabla ya mama kupatiwa huduma hiyo, huwa anapatiwa elimu kuhusu mtiririko wa huduma hiyo na pia huduma hiyo ni salama kwa mama na mtoto atakeyezaliwa.