Dodoma jiji FC yapata ajali basi lapinduka mara mbili

By Halfani Chusi , Nipashe
Published at 12:44 PM Feb 10 2025
Dodoma jiji FC yapata ajali basi lapinduka mara mbili.
Picha:Mtandao
Dodoma jiji FC yapata ajali basi lapinduka mara mbili.

Basi la timu ya Dodoma Jiji FC limepata ajali ya asubuhi hii maeneo ya Nangurukuru kuelekea Somanga mkoani Lindi likitokea mjini Ruangwa ambako jana walicheza mechi ya ya Ligi Kuu NBC dhidi ya Namungo FC.

Inaelezwa kuwa basi hilo lilipinduka mara mbili. Taarifa zinadai wachezaji wengi wamepata majeraha na hakuna kifo kilicho ripotiwa

Katibu Mkuu wa Timu hiyo, fortunatus Johnson amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo, na kwamba kwa sasa huduma ya uokozi inaendelea.