Mkurugenzi wa AICC ateuliwa Mjumbe wa Bodi ya Mamlaka ya Maji Arusha

By Cynthia Mwilolezi , Nipashe
Published at 04:08 PM May 21 2024

Picha ya kuunganisha ya Waziri wa Maji, Jumaa Aweso na Christine Mwakatobe.
Picha: Nipashe Digital
Picha ya kuunganisha ya Waziri wa Maji, Jumaa Aweso na Christine Mwakatobe.

WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amemteua Christine Mwakatobe kuwa mjumbe wa Bodi ya Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Arusha, (AUWSA) kuanzia Mei 13 mwaka huu.

Mwakatobe kwa sasa ni Mkurugenzi Mkuu wa Kituo Cha Kimataifa cha Mikutano Arusha AICC.

Sehemu ya barua ya uteuzi inaeleza  kuwa Waziri Aweso amemteua Mwakatobe, kwenye bodi hiyo nafasi ya mwakilishi wa watumiaji wakubwa wa maji jijini Arusha.

“Ni matarajio yangu kuwa utaupokea uteuzi na kufanya kazi kwa bidii na uadilifu ili Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Arusha, iendelee kutoa huduma bora na zenye viwango vya hali ya juu,” amesema Waziri Aweso

Katika  barua hiyo Aweso amenukuliwa na kusisitiza kuwa Mwakatobe atatekeleza majukumu yake, kwa kuzingatia miogozo na maelekezo ya Wizara, Msajili wa Hazina na Serikali.  

Kabla ya kuteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa AICC, Machi mwaka huu  Mwakatobe ambaye kitaaluma ni mchumi na mtaalamu wa masoko, alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa  Kampuni ya Uendelezaji na Uendeshaji wa Kiwanja cha Ndege cha Kilimanjaro 
KADCO.