Watuhumiwa sita akiwemo Katibu wa Chama cha Wamiliki Ardhi na Nyumba Tanzania (CHAWANYATA) Wilaya ya Temeke, Michael Kateka (68) wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Temeke Dar es Salaam mapema leo wakikabiliwa na mashtaka mawili likiwemo la kuvunja na kuiba vitu mbalimbali vyenye thamani ya zaidi ya Sh.milioni 31.
Washtakiwa Wengine ni Bilali Juma(32) Mkazi wa Mtoni na wakazi wa Magurumbasi ni Isiaka Kapemba(32),Hemed Kapemba(32), Fadhili Kapemba na mjumbe wa shina wa maeneo hayo,Hassan Kitigi.
Washtakiwa hao wamesomewa mashtaka yao na Wakili wa Serikali, Nicas Kihemba, mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo Ally Mkama.
Wakili Kihemba alidai katika shtaka la kwanza inadaiwa kati ya Novemba 2,2022 maeneo ya Keko Makurumbasi washtakiwa kwa pamoja walivunja na kuingia kwenye duka la Isack Mtenga.
Aidha Katika shtaka la pili inadaiwa tarehe na maeneo hayo washtakiwa kwa pamoja waliiba vitu mbalimbali vya dukani ikiwemo tairi saba za gari,vioo vya gari vya scania,dawa za ng'ombe ,nyaraka mbalimbali pamoja na spana moja mbavyo vina jumla ya thamani zaidi ya Sh milioni 31.
"Upelelezi umekamilka na ameiomba Mahakama hiiipange tarehe ya kuwasimea hoja za awali washtakiwa hao,"alidai Kihemba.
Washtakiwa hao walikana kutenda makosa hayo na kuomba dhamana.
Hakimu, Mkama alisema washtakiwa hao dhamana ipo wazi Kila mshtakiwa natakiwa awe na wadhamini wawili wawe na barua zinazotambulika kati ya hao mmoja anatakiwa atoe fedha taslimu kiasi cha Sh milioni 5 au hati yenye thamani hiyo na asaini bondi ya Sh milioni 5.
Washtakiwa wameshindwa kutimiza masharti ya dhamana na wamerudishwa hadi kesho kwa ajili ya kupata dhamana.
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED