WATU 13 wanadaiwa kufariki dunia na wengine sita kujeruhiwa katika ajali ya Basi dogo la abiria lililogongana uso kwa uso na roli la mafuta katika eneo la Somanga wilayani Kilwa.
Ajali hiyo imetokea leo Jumatatu Aprili 22, 2024 katika barabara kuu ya Somanga - Nangurukuru
Majeruhi hao wamepelekwa katika hospitali ya Tingi kwaajili ya matibabu zaidi na pia miili ya marehemu imehifadhiwa katika chumba cha maiti hospitalini hapo
© 2024 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED