Rais Samia amlilia Sam Nujoma

By Christina Mwakangale , Nipashe Jumapili
Published at 05:09 PM Feb 09 2025
Rais Samia Suluhu Hassan
Picha: Mtandao
Rais Samia Suluhu Hassan

RAIS Samia Suluhu Hassan, amesema amesikitishwa na taarifa ya kifo cha Baba wa Taifa la Namibia na Rais wa Kwanza wa taifa hilo, Sam Nujoma.

Ametuma salamu za rambirambi kwa Wanamibia kutokana na kifo hicho. 

Nujoma (95), amefariki dunia jana, jijini Windhoek nchini humo, akiwa ni miongoni mwa wapigania uhuru na wanaharakati wa ukombozi wa nchi za Kusini mwa Afrika, walioungwa mkono na Mwalimu Julius Nyerere.

Sam Nujoma
Rais Samia alisema: “Nimesikitishwa sana kupata habari za msiba wa Rais wa Kwanza na Baba Mwanzilishi wa Taifa la Jamhuri ya Namibia, Mheshimiwa Dkt. Sam Nujoma.

“Mpigania uhuru, Mwana-Pan-Africanist, na rafiki wa dhati wa Tanzania ambako aliwahi kuishi wakati wa harakati za uhuru wa Namibia.

Rais wa Namibia, Dk. Nangolo Mbumba, amesema nchi hiyo itatangaza maombolezo ya kitaifa.

Amesema Nujoma alifariki kutokana na maradhi yaliyokuwa yakimkabili baada ya kulazwa hospitalini kwa wiki tatu.