Nchini Myanmar, kuna matangazo yanayotoa motisha ya zaidi ya kati milioni 100 na manufaa mengine ukiolewa na mwanaume Mchina na kupata mtoto yanaenea katika mitandao ya kijamii.
Soko la wanaume wa China wanaotafuta wake wa Burma sio tu katika miji ya mpaka ya Uchina -Burma kama hapo awali, lakini pia huko Yangon. Imeenea katika miji mikubwa kama Mandalay.
Kuna wasiwasi kuwa, soko hili litakua zaidi baada ya video mbili za wasichana wenye umri mdogo mjini Yangon wakipewa wame wa kichina kusambaa kwenye mitandao ya kijamii.
"Wasichana wachanga kutoka familia zenye uhaba wa kifedha ambao wameolewa na kupata watoto wanakuwa walengwa wa madalali wa bibi harusi wa China," uchunguzi wa shirika la habari unafafanua.
Katika wiki ya kwanza ya Februari 2025, video mbili zilisambaa, zikidai " wanatafuta mke kwa ajili ya mwanaume Mchina huko Yangon."
Katika kipande kimoja cha video, sauti ya kiume inasema kwa Kichina, "Usiogope, ndugu yangu ni mtu mzuri," wakati mwanamke wa Burma, anayeaminika kuwa dalali anayezungumza Kichina, akitafsiri.
Video hiyo inawaonyesha wasichana wawili wa Kiburma wa umri wa shule ya sekondari na mama yao wakishawishiwa na mwanamume Mchina na dalali kuwa wake wa China.
Uchunguzi katia eneo hilo, uligundua kuwa ilikuwa katika mkoa wa Yangon, mji wa Dala, Ilifahamika kuwa ilitokea katika kitongoji cha Kamakasit.
"Msichana mwenye umri wa kwenda shule alipatikana kupitia mtandao wa kijamii wa Uchina wa Tik Tok na raia wawili wa China na wakalimani wawili walifika nyumbani kwake," ofisa kutoka shirika la kutoa misaada lililoko Dala akamwambia mwanahabari.
"Walitumia matatizo yangu ya kifedha na kunipa pesa ili niwe mke Mchina," anasema katika.
Video hiyo, inaonyesha wasichana wawili waliovalia sare nyeupe za shule, huku Mchina akiwaambia wasichana hao kwa lugha yao, kwamba atawaoa kwa pesa, pia kuwataka wabadilishe nguo zao.
Picha za wasichana hao wawili na familia zao zimekuwa zikisambazwa kwenye mitandao ya kijamii ya China kama vile Douyin na TikTok.
Mnamo tarehe 6 Februari 2025, raia wawili wa China waliokuwa wakirekodi video hiyo walikamatwa kwenye uwanja wa ndege.
Matukio haya hayafanyiki Yangon pekee, bali pia katika baadhi ya hoteli huko Mandalay, zinazojulikana kama hoteli za Wachina, ambazo zimehusishwa na baadhi ya watu wenye asili ya Kichina.
Baadhi ya madalali wanazurura katika hoteli za Wachina wanadaiwa na inasemekana madalali hupanga wanawake wa Burma wakutane na wanaume wa China wanaotaka kuwaoa.
Inadaiwa kuna mwanamke ambaye alishawishiwa kwa kisingizio cha uongo kufanya kazi na kuwa mke wa Kichina
Katika soko la bibiharusi la Uchina, wanawake walioolewa ambao wamezaa watoto wanaongoza kwa viwango vya juu zaidi vya malipo kwa madalali, anasema dalali wa Mandalay Ma Zar Chi.
"Wachina wanataka tu kupata watoto, kwa hivyo hawahitaji kuwa wazuri. Watu ambao wamepata watoto wana uwezekano mkubwa wa kupata wanaume. Mara nyingi madalali hupata watu ambao wamepata watoto," anaelezea Ma Zar Chi.
Anasema kuwa mwanamke ambaye amejifungua chini ya umri wa miaka 30 anaweza kupata hadi Yuan 100,000 (karibu Kyati milioni 600) kutoka kwa madalali na wanaume wa China.
Wasichana walio na umri mdogo hulipwa gharama kubwa zaidi, wakigharimu kati ya Yuan 100,000 na 150,000.
Lakini bei hizi hutolewa moja kwa moja kwa madalali na ni kiasi ambacho wale wanaoweza kumudu wanaweza kumudu. Dalali Ma Zar Chi alieleza.
BBC inatajwa kugundua kuwa wasichana wa Myanmar wanapotolewa kuwa wake wa China, madalali huwapa zaidi ya milioni moja pekee.
"Kwa sababu kuna viwango vingi vya madalali, wanagawana faida, na wasichana ambao wanakuwa wake wanapata mia chache tu," wakala Ma Zar Chi alielezea.
Tunapofuatilia soko la bibi harusi la Kichina, tunaona mifumo mitatu.
Imebainika kuwa kuna watu wengi wanaofanya kazi na madalali ili kuwa wake wa China kutokana na mahitaji ya kifedha, huku wengine wakidanganywa kufanya kazi katika viwanda nchini China na kisha kuuzwa kama wake wa China.
Kyi Pyar, mwanamke mwenye umri wa miaka 27, alishawishiwa kwenda kwenye kiwanda cha nguo cha China kwa ahadi ya kupata zaidi ya kyati milioni moja (kama Yuan 2,000 za Kichina) kwa mwezi na kisha kuuzwa kama mke wa China.
"Nilipewa mshahara mzuri na ofa ya kazi kutoka China iliyoandikwa kwa herufi za Kichina. Ningeweza kuondoka baada ya miezi mitatu au minne," Ma Kyi Pyar alisema, akiamini ombi la wakala huyo na kulikubali.
·Kwa mujibu wa BBC
© 2025 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED