Rais Samia akutana na Rais wa China, asaini makubaliano ya kuboresha reli ya TAZARA

By Mwandishi Wetu , Nipashe
Published at 04:35 PM Sep 04 2024
Rais Samia akutana na Rais wa China, asaini makubaliano ya kuboresha reli ya TAZARA
Picha:Ikulu
Rais Samia akutana na Rais wa China, asaini makubaliano ya kuboresha reli ya TAZARA

Rais Samia Suluhu Hassan amefanya kikao na Rais wa China, Xi Jinping wamejadiliana kuimarisha uhusiamo mzuri uliodumu zaidi ya miaka 60.

Rais Samia alikutana na  Rais Jinping pamoja na ujumbe wake mapema leo katika ukumbi wa The Great Hall of the People jijini Beijing. 

Aidha, Rais Samia  amefanikiwa kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia ya Tanzania na nchi muhimu duniani ikiwepo China tangu alipoingia madarakani mwaka 2021. 

Baada ya kikao hicho Rais Samia,  Rais Jinping na Rais wa Zambia  Hakainde Hichilema, walishuhudia uwekaji saini wa hati ya makubaliano ya kuboresha reli ya TAZARA.