HALI ya utulivu imeanza kurudi katika mji mkuu wa Kenya na maeneo mengine nchini Kenya kufuatia maandamano ya kupinga ongezeko la kodi na ushuru.
Biashara na maduka yamefunguliwa huku wananchi wakiripotiwa kuendelea na shughuli zao za kawaida.
Maandamano hayo yaliyoongozwa na vijana yalizuka wiki hii baada ya bunge la kitaifa kuupitisha mswada tata wa fedha uliotoa mapendekezo ya kuongeza ushuru.
Kufuatia maandamano hay Rais wa Kenya William Ruto alisema hatoutia saini mswada huo wa fedha na kutaka ufanyiwe marekebisho.
© 2024 IPPMEDIA.COM. ALL RIGHTS RESERVED