Watanzania washiriki mazoezi ili kuepuka magonjwa yasiyoambukiza
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa, jana alishiriki mazoezi ya pamoja ya kampeni ya kitaifa inayoratibiwa na Wizara ya Afya ya kuhamasisha Watanzania kufanya mazoezi ili kujiepusha na magonjwa yasiyoambukiza kama vile shinikizo la damu, maradhi ya moyo na kisukari.