Live updates

Mwanafunzi afariki kwa kugongwa na gari, wananchi wafunga barabara

Ida Mushi
Mwandishi
Ajali Morogoro
Picha:Ida Mushi
Ajali Morogoro
WANANCHI wa Kijiji cha Tabu Hotel wamefunga barabara kuu ya Dodoma-Morogoro tangu majira ya saa 11 wakishinikiza kufika Mkuu wa Mkoa wa Morogoro bwana Adam Malima baada ya gari ya serikali aina ya Cruzer kumgonga mwanafunzi kwenye kivuko cha watembea kwa miguu na kusababisha kifo chake na gari husika kukimbia.

Wanasema hawataki alama peke yake wanataka matuta kwasababu ajali eneo hilo zimekuwa za mara kwa mara zikihusisha magari ya Serikali zikiua wananchi wakiwemo wanafunzi.


DC Makame awatuliza wananchi, kesho TANROADS kujenga matuta

Ida Mushi
Mwandishi

Hatimaye wananchi wa Kijiji cha Tabu Hotel waliokuwa wamefunga barabara wameondoa vizuizi na magari yameruhusiwa kuendelea na safari baada ya Mkuu wa Wilaya ya Gairo,Jabir Makame kuingilia kati na kuwaahidi wananchi kuwa matuta makubwa yatajengwa Kesho Oktoba 25, 2024.

DC Makame afika eneo la tukio kuwatuliza wananchi

Ida Mushi
Mwandishi
news
Picha: Maktaba.
Mkuu wa Wilaya ya Gairo Jabiri Makame.

DC Makame amefika eneo la tukio na kuwaomba wananchi kuondoa vizuizi na wamekubali ili magari yapite.

Wananchi wamesema wanataka matuta katika eneo hilo

Ida Mushi
Mwandishi
Ajali Morogoro

Wanasema hawataki alama peke yake wanataka matuta kwasababu ajali eneo hilo zimekuwa za mara kwa mara zikihusisha magari ya Serikali zikiua wananchi wakiwemo wanafunzi.

Mwanafunzi aliyefariki anaitwa Yulia Samson Difrata mwanafunzi wa KIDATO Cha kwanza katika shule ya Sekondari Chigela, walikuwa watatu wengine wakawahi kurudi nyuma.

Wananchi washinikiza RC Malima kufika eneo la tukio

Ida Mushi
Mwandishi
news
Picha:Mtandao
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Adam Malima.

WANANCHI wa Kijiji cha Tabu Hotel wamefunga barabara kuu ya Dodoma-Morogoro tangu majira ya saa 11 wakishinikiza kufika Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Adam Malima baada ya gari ya serikali aina ya Cruzer kumgonga mwanafunzi  kwenye kivuko cha watenbea kwa miguu na kusababisha kifo chake na gari husika kukimbia.