Live updates

Matukio Mgomo wa Wafanyabiashara Tanzania

Frank Monyo
Mwandishi
Maduka yakiwa yamefungwa mkoani Arusha leo.
Picha: Getrude Mpyeza
Maduka yakiwa yamefungwa mkoani Arusha leo.
Jana Mwenyekiti Jumuiya ya Wafanyabiashara Kariakoo, Martin Massawe, alisema kuwa TRA imekubali kuboresha mfumo wake wa forodha na hivyo kamata kamata ya wafanyabiashara haitokuwepo tena, na kuwaomba wafanyabiashara wote waliofunga maduka wayafungue kwani serikali tayari imeshasikia kilio chao.

Lakini Leo Juni 26, 2024 Wafanyabiashara sehemu mbalimbali nchini wameendelea na mgomo kwa kutofungua maduka wakisubiri seeikali kutatua changamoto zao.

Mwenyekiti Wafanyabiashara: Uamuzi ni wenu kufunga au kufungua maduka

Frank Monyo
Mwandishi
Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Karikaoo, Martin Mbwana

Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Karikaoo, Martin Mbwana amewaachia uamuzi wafanyabiashara wa kufunga ama kufungua maduka yao, baada ya kuwapatia mrejesho wa kile kilichozungumzwa katika kikao baina ya viongozi hao na Serikali.

Wafanyabiashara Iringa nao wafunga maduka

Mwandishi Wetu
Mwandishi
news
Pocha: Mpigapicha Wetu
Wafanyabiashara Iringa nao wafunga maduka

Wafanyabiashara mkoani Iringa wamefunga maduka yao leo Juni 26/2024 ikiwa ni muendelezo wa mgomo unaofanywa na wafanyabiashara mbalimbali nchini.

Wafanyabiashara Iringa nao wafunga maduka.

Mduka zaidi ya fungw

Mwandishi Wetu
Mwandishi
news
Picha: Mpigapicha Wetu
Mduka zaidi ya 500 yafungwa Tunduma

ZAIDI ya maduka 500 katika Soko la Manzese pamoja na Soko Kuu la Halmshauri ya Mji Tunduma yaliyopo katikati ya Mji wa Tunduma mkoani Songwe yamefungwa na kusababisha adha kwa wanunuzi wa bidhaa.

Mwenyekiti Wanyabiashara Arusha atoa kauli

Getrude Mpezya
Mwandishi
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Jijini Arusha, Loken Adolf.

Wafanyabiashara Arusha wafunga maduka yao

news
Picha: Getrude Mpezya
Wafanyabiashara Arusha wafunga maduka

Wafanyabiashara katika eneo la mjini kati jijini Arusha wamefunga maduka yao ikiwa ni mgomo ambao wanaufanya kwa madai mbalimbali ambayo bado hawajayaweka wazi.

Kulingana na baadhi ya Wafanyabiashara hao wanasema jana Juni 25, 2024, vipeperushi vilisambazwa kwenye maduka yao kupitia baadhi ya vijana vikihamasisha kufungwa kwa biashara kwa muda wa siku mbili.