Live updates

Rais Samia amefanya uteuzi na utenguzi kwa viongozi

Frank Monyo
Mwandishi
Rais Samia Suluhu Hassan.
Picha: Ikulu
Rais Samia Suluhu Hassan.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi, utenguzi na uhamisho wa viongozi kama ifuatavyo:

Uteuzi huu na utenguzi ameufanya usiku wa Leo Jumapili Machi 31,2024.

Rais Samia amempeleka Kundo Mathew kuwa Naibu Waziri Maji

Frank Monyo
Mwandishi
news
Picha: Maktaba.
Kundo Andrea Mathew.

Rais Dk. Samia Suluhu Hassan amemhamisha Kundo Andrea Mathew kutoka kuwa Naibu Waziri Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kwenda kuwa Naibu Waziri wa Wizara ya Maji. 

Samia amemteua Daniel Sillo kuwa Naibu Waziri Mambo ya Ndani

Frank Monyo
Mwandishi
news
Picha: Maktaba.
Daniel Baran Sillo.

Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amemteua Daniel Baran Sillo, kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi.

Sillo anachukua nafasi ya Jumanne Abdallah Sagini ambaye amehamishwa kwenda kuwa Naibu Waziri wa Wizara ya Katiba na Sheria

Rais Samia amteua Zainab Katimba, Naibu Waziri TAMISEMI

Frank Monyo
Mwandishi
news
Picha: Maktaba.
Zainab Athuman Katimba.

Mbunge wa Viti Maalum Zainab Athuman Katimba, ameteuliwa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kuwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Tawala za Mikoa ana Serikali za Mitaa (TAMISEMI).


Anachukua nafasi ya Deogratius John Ndejembi ambaye ameteuliwa kuwa Waziri. 

Rais Samia amemteua Kanali Mtambi RC Mara

Frank Monyo
Mwandishi
news
Picha: Maktaba.
Kanali Evans Alfred Mtambi.

Wakati huo aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Mkinga Kanali Evans Alfred Mtambi, ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara. 

Rais Samia amteua Said Mtanda Mkuu wa Mkoa Mwanza

Frank Monyo
Mwandishi
news
Picha: Maktaba
Said Mohamed Mtanda.

Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara Said Mohamed Mtanda, amehamishwa kwenda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, anachukua nafasi ya Amos Makalla ambaye atapangiwa kazi nyingine.

Prof. Ndalichako awekwa pembeni, Deo Ndejembi, kuwa Waziri OWM- Vijana

Frank Monyo
Mwandishi
news
Picha: Maktaba
Degratius John Ndejembi.

Aliyekuwa Naibu Waziri wa TAMISEMI Degratius John Ndejembi, ameteuliwa na Rais Dk. Samia Suluhu kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu).

Ndejembi anachukua nafasi ya Prof. Joyce Lazaro Ndalichako ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Makonda ateuliwa Mkuu wa Mkoa Arusha

Frank Monyo
Mwandishi
news
Picha: Maktaba.
Paul Makonda.

Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Paul Makonda kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha.


Kabla ya uteuzi huu Makonda alikuwa Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na anachukua nafasi ya John Mongella ambaye atapangiwa kazi nyingine.