Aliyoyasema Rais Samia kuhusu Sokoine liwe somo kwa viongozi
Juzi, taifa liliadhimisha kumbukizi ya miaka 40 tangu aliyekuwa Waziri mkuu, Edward Sokoine alipofariki dunia. Hafla ya kumbukumbu hiyo ambayo Rais Samia Suluhu Hassan alikuwa mgeni rasmi, ilifanyika nyumbani kwa kiongozi huyo shujaa, aliyetumikia taifa kwa uaminifu, Monduli Juu mkoani Arusha.