13 May 2008 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Kadhi Mkuu wa Zanzibar afariki dunia
 
2008-05-13 17:55:52
Na Radio One Habari

Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Ali Hatib Mlanzi amefariki dunia ghafla leo nyumbani kwake Jang`ombe mjini Zanzibar.
Taarifa kutoka Ofisi ya Waziri Kiongozi zimesema Sheikh Mlanzi amefariki dunia mapema asubuhi wakati akijiandaa kwenda kazini.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Kadhi Mkuu huyo hakuugua na amefariki dunia miaka miwili tangu ashike wadhifa huo.

Aidha taarifa hiyo imesema maziko ya marehemu tayafanyika leo saa kumi jioni katika makaburi ya Shakani wilaya Magharibi Unguja.

  • SOURCE: Radio One
Tuma Maoni Yako
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2007 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.