|
Wanaowafungia watoto walemavu washitakiwe
2008-05-11 20:03:26
Na Radio One Habari
Watu wenye ulemavu mkoani Rukwa wameiomba serikali kuwachukulia hatua za kisheria wazazi wenye tabia ya kuwafungia ndani watoto wenye ulemavu kwa kuhofia kuchekwa.
Ushauri huo umetolewa na umoja wa Chama cha Watu wenye Ulemavu-CHAWATA tawi la Sumbawanga wakati wakizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za chama hicho mjini Sumbawanga.
Katibu wa chama hicho kitengo cha wanawake Bi. Yasinta Chipeta amesema ushauri huo umefuatia utafiti walioufanya na kubaini kuwa kuna watu wengi ulemavu ambao wanafungiwa ndani na wazazi wao tangu wakiwa wachanga, kwa kuogopa kuchekwa na watu katika jamii zao.
Amesema vitendo hivyo ni ukiukwaji wa haki za binadamu na kwamba vimekuwa vikiwanyima fursa ya kupata haki elimu walemavu hao.
|