11 May 2008 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Wanaouza mafuta ya petroli na dizeli kinyume cha sheria kusakwa Z`bar
 
2008-05-11 20:00:45
Na Radio One Habari

Bodi ya Mapato Zanzibar-ZRB kwa kushirikiana na jeshi la polisi katika mkoa wa Mjini na Magharibi imeanzisha operesheni maalum kuwasaka wauzaji wa mafuta ya petroli na dizeli kinyume cha sheria katika manispaa ya Zanzibar.

Kamanda wa polisi wa mkoa huo Bwana Bakari Khatibu Shabani amesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Amesema polisi na bodi hiyo zimeanzisha operesheni hiyo kutokana na baadhi ya wafanyabiashara kuanzisha utaratibu wa kuuza bidhaa hiyo sehemu ambazo hazikubaliki kisheria na kuhatarisha maisha.

Kamanda Bakari amesema sababu nyingine ni kupambana na wafanybiashara ambao wanaikosesha serikali kodi inayotokana na uuzaji wa mafuta.

Amesema wafanyabiashara kadhaa wamekamatwa tangu kuanza oparesheni hiyo na kwamba itaendelea.

  • SOURCE: Radio One
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2007 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.