Swahilinews |
 |
NAVIGATION |
 |
|
 |
|
|
 |
SEARCH |
 |
|
|
|
 |
SPECIAL |
|
|
 |
|
|
 |
ARCHIVES |
|
|
 |
|
|
 |
|
 |
|
|
|
Uendeshaji wa Mashamba ya mpunga ya Kapunga uratibiwe
2008-05-10 19:26:52
Na Radio One Habari
Serikali imeombwa kuratibu uendeshaji wa mashamba ya mpunga ya Kapunga Mkoani Mbeya ambayo wamiliki wake wanataka kulima zao la mibono kwa ajili ya kuzalisha nishati ya kuendeshea mitambo badala ya kuongeza uzalishaji wa chakula nchini.
Wakizungumza baada ya kutembelea mashamba ya miwa ya Kilombero na bwawa la uzalishaji wa umeme la Kidatu, wajumbe wa Bodi ya maji ya Bonde la Rufiji wamesema hatua ya mwekezaji kubadili kilimo cha mpunga ambalo ni zao la chakula na kulima mibono kitapunguza upatikanaji wa chakula.
Makamu mwenyekiti wa bodi bwana Abed Mwasajone amepinga uamuzi huo na kusisitiza kama mwekezaji ameshindwa kulima mpunga serikali ichukue mashamba hayo na kugawa kwa wananchi.
Hoja hiyo iliungwa mkono na mwenyekiti wa bodi hiyo bwana Bakari Mbonde ambae amesema hatua hiyo itakuwa na athari kubwa kimazingira na mtiririko wa maji katika bonde la Ihefu na mto Ruaha mkuu.
Kwa siku za karibuni wadau mbalimbali wamekuwa wakitoa maoni kuwa ujio wa kilimo cha mazao yanayolenga kuzalisha nishati ya kuendeshea mitambo utaathiri uzalishaji wa chakula na hifadhi ya mazingira kwani kilimo hicho kitahitaji maeneo makubwa na kuhusisha ufyekaji wa misitu na mapori.
|
|
 |
Habari za Leo |
|
|
----------------------------------------------- |
Maoni ya Mhariri |
|
|
----------------------------------------------- |
Business
bits |
|
|
----------------------------------------------- |
Makala |
|
|
| |
 |
|