08 Feb 2008 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Liwale yapatiwa tani 145 za chakula kutoka serikalini
 
2008-02-08 17:09:38
Na Radio One Habari

Serikali imeipatia wilaya ya Liwale mkoani Lindi tani 145 za chakula aina ya wanga, kwa ajili ya kuwasaidia wananchi wanaokabiliwa na upungufu mkubwa wa chakula wilayani humo.

Kiasi hicho cha chakula ni kati ya tani 680 zinazohitajika, zikiwemo 618 za wanga na 62 za protini, ili kutosheleza mahitaji ya watu Elfu-10 Mia Tano 69 waliokumbwa na upungufu huo wa chakula kutoka vijiji 15 vya wilaya hiyo hadi kufikia Aprili mwaka huu.

Mkuu wa wilaya ya Liwale Bibi Anna Magowa, amesema chakula hicho kitauzwa kwa waathirika kwa bei ya shilingi 50 kwa kilo na kwamba tayari wilaya hiyo imeshapatiwa shilingi milioni 33 Laki Sita na Elfu-69 kwa ajili ya kusafirishia chakula hicho kutoka
Dar es Saalam.

Mkuu huyo wa wilaya alikuwa akitoa taarifa yake kwa mkuu wa mkoa wa Lindi Bwana Saidi Meck Sadiki alipotembelea wilaya hiyo kukagua maeneo yaliyokumbwa na upungufu wa chakula.

  • SOURCE: Radio One
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2007 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.