|
Auwa mkewe baada ya kuzuiwa kupiga mtoto
2006-07-16 19:08:16
Na Radio One Habari
Mkazi wa kijiji cha Kanazi wilayani Ngara, mkoani Kagera, Bwana Dedani Yona amemuua mke wake kwa kumpiga na kumkaba shingo baada ya mwanamke huyo kumzuia mumewe kumpiga mtoto wao.
Mwenyekiti wa kitongoji cha Kanazi, Bwana Michael Efta amemtaja mwanamke aliyeuawa kuwa ni Yudita Dedani na kwamba mauaji hayo yalitokea siku ya Alhamisi saa tatu usiku nyumbani kwa wanandoa hao.
Marehemu ameacha watoto watatu akiwemo mtoto mchanga mwenye umri wa miezi saba.
Dedani Yona pamoja na jirani yake mmoja wanashikiliwa na polisi wilayani Ngara ambapo jirani huyo anaisaidia polisi kwa sababu aliwahi kufika kwenye eneo la tukio wakati ugomvi ukiendelea.
|