16 Jul 2006 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Shirika la nyumba kujenga maghorofa mikoani
 
2006-07-16 19:04:39
Na Radio One Habari

Shirika la Nyumba la Taifa linatarajia kumaliza tatizo la uhaba wa nyumba za kupanga nchini kwa kuongeza maghorofa mengine kwa kila mkoa.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi Bibi Salome Sijaona amesema hayo alipotoa maelezo kwa Rais Jakaya Kikwete mipango mbali mbali ya shirika hilo kwenye uwekaji wa jiwe la msingi kwenye ujenzi wa maghorofa mawili ya shirika hilo yaliyopo katika eneo la Mpwapwa Mafleti Mkoani Dodoma.

Maghorofa hayo yenye ghorofa nne yatakuwa na uwezo wa kuchukua familia 24 na yatagharimu Shilingi Bilioni 1.88 na yatakamilkka mapema Februari mwakani.

Bibi Sijaona amesema shirika lina majengo mengi kwenye maeneo muhimu kati kati ya miji ya nchi, lakini majengo mengi yamechakaa na mengine yamepitwa na wakati na hivyo hayastahili kuwepo katik kati ya mji.

Amesema kutokana na tatizo hilo shirika limewashirikisha wawekezaji wengine wenye uwezo ili kuendeleza maeneo hayo ya kati ya miji kwa kuvunja majengo yaliyopo na kujenga majengo makubwa zaidi.

  • SOURCE: Radio One
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2005 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.