|
Rais Museven na Joseph Kabila kutua Dar leo
2008-05-11 19:51:25
Na ITV Habari
Rais Yoweri Museveni wa Uganda na Rais Joseph Kabange Kabila wa Jamhuri ya kidemokrasi ya Kongo watawasili Dar es Salaam leo kwa mwaliko wa rais Jakaya Kikwete.
Taarifa kutoka wizara ya mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa imesema wakati wa ziara hiyo, viongozi hao watakuwa na majadiliano kuhusu masuala yanayohusu amani katika eneo la nchi za maziwa makuu na mambo mengine yanayozihusu nchi zao.
Marais hao wawili wanatarajia kuondoka leo baada ya kukamilisha ziara yao.
|