11 May 2008 MAIN PAGE SITE INDEX CONTACT US HELP
  Swahilinews
NAVIGATION
SEARCH
 
SPECIAL  
ARCHIVES  
Print this article Send this article

Laston ateuliwa kuwa katibu mkuu katika wizara ya fedha na uchumi
 
2008-05-11 19:46:59
Na ITV Habari

Rais Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Laston T. Msongole kuwa naibu katibu mkuu katika wizara ya fedha na uchumi.

Taarifa iliyotolewa leo Ikulu, Dar es Salaam na katibu mkuu kiongozi, Bw. Philemon Luhanjo imesema uteuzi huo unaanza mara moja ambapo Bw. Msongole atashughulikia masuala ya uchumi na bajeti katika wizara hiyo.

Kabla ya uteuzi wake, Msongole alikuwa mkurugenzi wa masuala ya uchumi katika iliyokuwa wizara ya mipango, uchumi na uwezeshaji.

Wizara hiyo ilifutwa katika mabadiliko ya muundo mpya wa serikali uliotangazwa na Rais Kikwete Februari mwaka huu.

  • SOURCE: ITV
Habari za Leo
-----------------------------------------------
Maoni ya Mhariri
-----------------------------------------------
Business bits
-----------------------------------------------
Makala
 
Privacy Statement Terms Of Use ©1998-2007 IPPMedia Ltd.  All Rights Reserved.