|
Chuo kikuu Dar waelezea kifo cha mwanafunzi aliyefia bwawani
2008-05-10 18:10:04
Na ITV Habari
Uongozi wa chuo kikuu cha Dar es Salaam umesema taarifa zilizopo chuoni hapo zinaonyesha mwanafunzi Deogratias Dominick alikufa katika bwawa la kuogelea chuoni hapo wakati wa vurugu zilizokuwa zimetokea chuoni siku ya tarehe 22 mwezi Februari mwaka huu.
Akizungumza na ITV ofisini kwake makamu mkuu wa chuo mipango fedha na utawala profesa Yunus Mgaya amesema ripoti ya ukaguzi wa awali wa mwili wa marehemu imeonyesha kwamba mwanafunzi huyo alikufa kabla ya kufikishwa hospitali na hakuwa na jeraha sehemu yoyote ya mwili wake.
|