|
Mtwara na Lindi waomba wafugaji waendelea kuhamia kwao
2008-05-10 18:08:57
Na ITV Habari
Wadau wa mifugo wa mikoa ya Mtwara na Lindi wameiomba serikali, kuendelea kuwahamasisha wafugaji hasa wa ng`ombe, kupeleka mifugo yao mikoa ya Kusini, pia kuanzisha viwanda vya kusindika nyama ili kukuza biashara ya mifugo, kutokana na mikoa hiyo kuwa nyuma katika shughuli za ufugaji.
Wadau hao wametoa maombi hayo kwenye warsha iliyoandaliwa na wizara ya mifugo na uvuvi, yenye lengo la kuandaa mkakati wa kutekeleza sera ya taifa ya mifugo ya mwaka 2006 ambapo wamesema uchache wa mifugo na madawa ya kutibu maradhi, umesababisha bei ya nyama kwa walaji kuwa kubwa.
Hata hivyo mtaalamu wa kilimo toka chuo kikuu cha kilimo - SUA -cha Morogoro Prof. Lusato Kuligila amesema changamoto inayowakabili wafugaji wa mikoa ya kusini, ni upatikanaji wa mifugo bora na udhibiti wa magonjwa.
|