|
Benki za biashara nchini zimetakiwa kusambaza huduma vijijini
2008-05-08 14:34:04
Na ITV Habari
Benki za biashara nchini zimetakiwa kuonesha kwa vitendo uwezo wake wa kupanua wigo wa huduma zao kwa watanzania kwa kupeleka huduma zao kwenye mikoa na wilaya na vijijini badala ya kung`ang`ania miji mikubwa yenye biashara na shughuli nyingi za kiuchumi.
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Bw. Yohana Balele amesema hayo wakati akizindua tawi la benki ya Posta mkoani humo ambapo mkurugenzi mtendaji wa benki hiyo Bw. Alphonce Kihwele amesema uzinduzi huo ni katika mipango ya kusambaza huduma zake kuweza kufikia watanzania walio wengi zaidi.
|