|
Madiwani waelezea kusikitishwa na taarifa ya halmashauri
2008-05-07 11:31:54
Na ITV Habari
Baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Ulanga mkoani Morogoro limeitaka wizara ya tawala za mikoa na serikali za mitaa kuwachukulia hatua watumishi wa halmashauri hiyo walioanzisha vyanzo binafsi vyamapato nakukusanya fedha kwa kutumia stakabadhi za halmashauri .
Wakizungumza katika kikao cha baraza hilo kilichohudhuriwa na mkuu wa wilaya hiyo Dr. Rajab Rutengwe madiwani hao wameelezea kusikitishwa na taarifa ya halmashauri iliyoonesha hadi 2008 halmashauri ilikusanya asilimia 42 za mapato yote ya mwaka 2007/2008 kiasi cha shilingi milioni 184.
|